You are here

Back to top

N'Na Kwetu: Sauti ya Mgeni Ugenini (Paperback)

N'Na Kwetu: Sauti ya Mgeni Ugenini Cover Image
$16.00
Usually Ships in 1-5 Days
(This book cannot be returned.)

Description


DIWANI hii ya N'na Kwetu: Sauti ya Mgeni Ugenini ilishinda kwenye awamu ya kwanza ya Tuzo za Fasihi ya Afrika kwa Lugha ya Kiswahili inayotolewa na Wakfu wa Mabati-Cornell mwaka 2015. Tungo nyingi zilizomo humu ziliandikwa baina ya robo ya mwisho ya mwaka 2010 na nusu ya mwanzo ya mwaka 2015. Hii ni miaka mitano ya mwanzo ya mshairi kuhamia na kuishi nchini Ujerumani - mbali na nyumbani kwao, Zanzibar. Ndani yake, kwa hivyo, muna muakisiko wa hisia za mgeni ugenini, akitayamani mengi mazuri ya kwao na akijutia kuyaacha nyuma yake. Ukweli ni kuwa wakati mtu anapoishi ugenini, ndipo hasa ile thamani ya kwao anapoitambua na kutaka kujitambulisha nayo zaidi na zaidi. Ndipo hisia za kutambuwa kuwa ana kwao zinapopanda kiwango cha juu. Kutoka kipembe cha mbali, Mohammed Ghassanani anakuangalia kwao na kuyaona mambo ambayo alipokuwamo ndani yake, alikuwa hata hajui kama yapo. Chembilecho Wajapani: "Samaki hajijui kuwa amerowa " Na sababu ya kutokujijuwa huko, kwa hakika, ni kwa kuwa yeye mwenyewe anaishi ndani ya maji muda wote.

Product Details
ISBN: 9781470942892
ISBN-10: 1470942895
Publisher: Lulu.com
Publication Date: September 27th, 2021
Pages: 126
Language: Swahili